Psalms 100

Dunia Yote Yaitwa Kumsifu Mungu

(Zaburi Ya Shukrani)

1 aMpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.

2 bMwabuduni Bwana kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.

3 cJueni kwamba Bwana ndiye Mungu.
Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake;
sisi tu watu wake,
kondoo wa malisho yake.


4 dIngieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.

5 eKwa maana Bwana ni mwema
na upendo wake wadumu milele;
uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Copyright information for SwhKC